Thursday, February 23, 2012

BIASHARA NDOGO NDOGO NA UJASIRIAMALI

UJASIRIAMALI na BIASHARA NDOGO NGOGO
Watu wengi wamekuwa wakitumia neno Mjasiriamali kama mfanya biashara ndogondogo, kuna uhusiano baina ya ufanyaji biashara ndogo ndogo na Ujasiriamali, lakini hakuna usawa kati ya vitu hivi viwili kwa dhana zifuatazo:

Kiasi cha Fedha na Utajiri.

Mfanya biashara ndogo ndogo mara nyingi hulenga kujipatia kipato cha kujikimu kutokana na ukosefu wa kazi ya kuajiriwa au ugumu wa maisha na maisha huwa hayana matarajio makubwa sana.
Mjasiriamali hufanya biashara au shughuli yake kwa malengo na matarajio ya kujipatia kipato cha kutosha kujikimu, kufanya mambo ya maendeleo na hatimaye kuwa tajiri Mkubwa kwa kuwekea mkazo shughuli zake kwa misingi muhimu ya maendeleo.

Malengo na muda wa Mafanikio
Mfanya biashara ndogondogo anaweza maliza muda mrefu, hata maisha yake yote ikibidi kwa kujipatia kipato kidogo sana, wakati Mjasiriamali huwa na ari na kasi ya ya shughuli yake kwa kuwa na malengo na kuyaendea kwa kasi hiyo ili kupata mafanikio na kujitengenezea utajiri ndani ya muda Fulani mfano ndani ya miaka 3.

Hatari za kibiashara na kuziendea mbio nafasi.

Mjasiriamali huangalia hatari zinazoikabili biashara au shughuli yake na kuwa na tahadhari za kutosha kujiepusha na madhara yanayoweza kuepukika ili azidi kusonga mbele, pia huzitolea macho fursa zinazopita mbele yake au kwa wengine na ku improvise(kuzinadia kwa upande wake) kwa mfanya biashara ndogo ndogo wa kawaida hili halimshughulishi sana ili mradi anauza kidogo, na chakula kinapatikana basi siku zinaenda.

Uvumbuzi na Ubunifu.
Mjasiriamali hufanya Uvumbuzi na Ubunifu zaida ya mfanya biashara ndogondogo wa kawaida, uvumbuzi huu humpa changamoto zenye faida ambazo hupelekea kutajirika, Uvumbuzi huu huwa katika bidhaa au huduma husika au katika utaratibu wa kibiashara katika kufikisha kwa wateja/watumiaji wake.

Mnaonaje Ndugu zangu?, huu ni mtazamo wa kisomi wa Kijasiriamali.

2 comments:

  1. Nisawa japo hii ni dhana ya mjasiriamali
    Siyo maana ya UJASIRIAMALI
    Neno ambalo lilianza miaka ya 1700 huko Amerika

    ReplyDelete
    Replies
    1. Tupe maana halisi jinsibya kujikimu na mfani wa biashara ndogo na masoko yake yanapo patikana

      Delete